• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China na Ureno zakubaliana kusukuma mbele ujenzi wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja"

    (GMT+08:00) 2018-12-06 09:45:32

    Rais Xi Jinping wa China amekutana na waziri mkuu wa Ureno Bw. Antonio Costa na kufikia makubaliano naye kuhusu kusukuma mbele ujenzi wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja" ili kuongeza mawasiliano kati ya Asia na Ulaya na kuhimiza biashara ya kimataifa.

    Rais Xi amesema China inapenda kushirikiana na Ureno kuimairsha uhusiano wa wenzi wa kimkakati kati yao.

    Kwa upande wake Bw. Costa amesema, Ureno inashukuru misaada inayotolewa na China katika kudumisha utulivu wa kiuchumi nchini humo, na kuwa Ureno inapenda kutumia fursa hii kushirikiana na China kuendeleza uhusiano wa pande mbili.

    Rais Xi pia alikutana na kufanya mazungumzo na spika wa bunge la Ureno Bw. Eduardo Ferro Rodrigues mjini Lisbon.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako