Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amesema ufisadi unagharimu dola za kimarekani trilioni 2.6, ikiwa ni sawa na asilimia 5 ya pato la dunia. Kwenye taarifa aliyotoa kabla ya Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Ufisadi, inayoangukia Disemba 9 kila mwaka, Bw. Guterres amesema kwa mujibu wa Benki ya Dunia, ukwepaji kodi, utakatishaji fedha na shughuli nyingine haramu zimehamisha rasilimali zinazohitajika kwa ajili ya maendeleo endelevu, na makampuni na watu binafsi hutoa rushwa zaidi ya dola za kimarekani trilioni moja kila mwaka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |