• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yahimiza ushirikiano wa kilimo kati yake na Zimbabwe

    (GMT+08:00) 2018-12-06 18:46:32

    Ofisa wa ubalozi wa China anayeshughulikia masuala ya uchumi nchini Zimbabwe Bw. Chen Ning amefanya sherehe ya kukaribisha timu ya wataalamu wa kilimo wa China watakaotoa mafunzo ya kilimo nchini Zimbabwe.

    Kwenye sherehe hiyo, Bw. Chen amesema, ni lazima kuhimiza ushirikiano wa kilimo kati ya China na Zimbabwe ili kuboresha zaidi sekta ya kilimo nchini Zimbabwe.

    Katibu wa kudumu wa Wizara ya ardhi, na kilimo wa Zimbabwe Bw. Ringson Chitsiko amewashukuru wataalamu wa China na kuhimiza wazimbabwe kujitahidi kupata mafunzo na ufundi ili kutoa mchango wao kwa maendeleo ya nchi yao.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako