Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeshindwa kupitisha muswada wa azimio uliotolewa na Marekani kukosoa mashambulizi ya roketi yaliyofanywa na kundi la Hamas dhidi ya Israel. Muswada huo ulipigiwa kura 87 za ndio, kura 57 za hapana na kura 33 hazikupigwa, na kushindwa kupitishwa kutokana na kura za ndio kutofikia theluthi mbili ya kura zote. Nchi zote za kiarabu ziliukataa muswada huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |