• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • IAAF yaingezea kibano Urusi hadi 2019 

    (GMT+08:00) 2018-12-07 10:14:21
    Rais wa shirikisho la kimataifa la riadha (IAAF) Lord Sebastian Coe, amesema wameiongezea adhabu ya Urusi kwa wanariadha wake kutoshiriki mashindano yoyote ya kimataifa hadi mwakani.

    Coe amesema kuwa IAAF ilitaka ipewe sampuli ya vipimo kutoka wakala wa kupiga vita matumizi ya dawa zilizopigwa marufuku michezoni (WADA) kutoka Urusi lakini nchi hiyo haikutekeleza.

    Ameeleza kuwa, kutokana na muda waliotoa kwa nchi hiyo kuwasilisha sampuli hizo kumalizika licha ya kuwakumbusha mara kadhaa wameona ni vyema adhabu hiyo iendelee.

    Russia ambao wanariadha wake hawajashiriki mashindano yoyote tangu mwaka 2016 wataendelea kukaa benchi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako