Vikosi vya Misri vimeanza mazoezi ya kijeshi ya pamoja ya kupambana na ugaidi na nchi washirika wa Afrika Sudan, Nigeria na Burkina Faso, ambazo ni nchi za kundi la kwanza kutoka Jumuiya ya Nchi za Sahel Sahara kushiriki kwenye mazoezi hayo. Mazoezi hayo yamefanyika katika kambi ya kijeshi ya Mohamed Naguib ambayo ni kubwa zaidi katika eneo la Mashariki ya Kati na Afrika na yataendelea mpaka Disemba, 14.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |