Idara ya kukabiliana na matukio ya dharura ya Nigeria imethibitisha kuwa miili ya watu 15 imepatikana na watu wengine 31 wameokolewa kutoka kwenye kifusi cha jengo la ghorofa saba lililobomoka mwezi uliopita mjini Port Harcourt, kusini mwa Nigeria.
Mratibu wa Idara hiyo Bw. Ejike Martins amesema umaalumu wa ajali hiyo ni kuwa ghorofa moja ilianguka moja kwa moja juu ya ghorofa nyingine, ndiyo maana kifusi kinaweza tu kuondolewa hatua kwa hatua.
Jengo hilo lililoko kwenye Eneo la Serikali mjini Port Harcourt lilianguka wiki tatu zilizopita wakati ujenzi unaendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |