Mkutano wa kati ya serikali wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhamiaji wa kimataifa umemalizika mjini Marrakech, Morocco. Mkutano huo wa siku mbili umeshuhudia kupitishwa rasmi kwa Mkataba wa Kimataifa wa Uhamiaji Salama, Wenye Utaratibu na wa Kawaida na nchi zaidi ya 150. Akikutana na waandishi wa habari, mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhamiaji wa kimataifa Louise Arbour amesema mkutano huo ni jambo la kihistoria kwa uhamiaji na sera ya ushirikiano wa pande nyingi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |