Shirika la ndege la Rwanda RwandAir litatumia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Ghana mjini Accra kufanya safari zake za kwenda Marekani.
Shirika hilo linasubiri kupata idhini husika kutoka kwa serikali ya Marekani ili kuanza safari hizo.
Mkurungezi mkuu wa RwandAir Yvonne Makolo amesema Accra itakuwa ndio kituo cha uunganishaji wa safari zote za Afrika kwenda Marekani.
Awali shirika la RwandAir lilipanga kuanza safari zake Juni 2019, na ilitarajia idhini zote kutolewa kabla ya mwezi Machi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |