Wizara ya biashara ya China imesema, China na Marekani zinafanya mazungumzo kuhusu mambo halisi ili kuhimiza mazungumzo ya kibiashara kati yao.
Msemaji wa wizara hiyo Bw. Gao Feng amesema China inakaribisha ujumbe wa Marekani kutembelea China na kufanya majadiliano, na inapenda kutuma ujumbe Marekani kufanya mazungumzo.
Msemaji huyo pia amesema nchi hizo mbili zimefikia makubaliano kuhusu masuala kadhaa yakiwemo bidhaa za kilimo, nishati na magari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |