Rais Xi Jinping amesema China inapaswa kuendelea kutoa kipaumbele katika maendeleo, ili kuongeza nguvu ya taifa, kushughulikia vizuri pengo kati ya mahitaji ya maisha bora ya wananchi na hali ya kutokuwepo kwa maendeleo yenye uwiano na ya kutosha, kubadilisha njia ya maendeleo kwa hatua madhubuti na kuboresha muundo wa uchumi, kutekeleza mkakati wa kuhimiza maendeleo kupitia uvumbuzi, na kuimarisha ujenzi wa mazingira.
Rais Xi Jinping amesema, sera ya mageuzi na kufungua mlango inapaswa kuzingitia zaidi mambo ya wananchi, na kuendana na matumaini yao, kuheshimu maoni yao, kufuatilia hali zao, na kushugulika na kazi za kuboresha maisha yao.
Rais Xi Jinping amesema China haiwezi kupata maendeleo kama ikijitenga na dunia, na ustawi wa dunia pia hauwezi kupatikana bila China. China inapaswa kushikilia kufungua mlango zaidi, na kuhimiza ujenzi wa jumuiya yenye mustakbali wa pamoja. Amesema, China itahimiza kujenga uhusiano mpya wa kimataifa wenye haki na usawa na wa kuheshimiana, kushirikiana ili kupata mafanikio ya pamoja, kuheshimu haki ya watu wa nchi nyingine ya kuchagua njia ya kujiendeleza, kusaidia nchi zinazoendelea kupata maendeleo, kuunga mkono utaratibu wa biashara wa pande nyingi, na kuanzisha majukwaa mapya ya kimataifa ya ushirikiano haswa pendekezo la "Ukanda Mmoja, Njia Moja".
Rais Xi Jinping amesema China inapaswa kushughulikia vizuri uhusiano kati ya mageuzi, maendeleo na utulivu, na China ni nchi kubwa ambayo haitakiwi kufanya makosa makubwa katika masuala kuu. Ameagiza kuhakikisha hatua kubwa za mageuzi zinatekelezwa kihalisi, na kuunganisha juhudi za kuhimiza mageuzi, maendeleo na utulivu.
Rais Xi Jinping amesema China inapaswa kushughulikia vizuri uhusiano kati ya mageuzi, maendeleo na utulivu, na China ni nchi kubwa ambayo haitakiwi kufanya makosa makubwa katika masuala kuu. Ameagiza kuhakikisha hatua kubwa za mageuzi zinatekelezwa kihalisi, na kuunganisha juhudi za kuhimiza mageuzi, maendeleo na utulivu.
Kwenye mkutano huo Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China na baraza la serikali la China zimetoa tuzo ya urafiki ya mageuzi ya China kwa wageni 10, ili kuwashukuru kwa mchango wao wa kuhimiza mawasiliano na ushirikiano kati ya China na nchi za nje, na kushiriki na kuunga mkono mchakato wa mageuzi na kufungua mlango nchini China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |