Katika ujumbe wa pongezi kwa Rais Putin, Rais Xi amesema mwaka 2018 ulikuwa wenye mafanikio makubwa katika uhusiano kati China na Russia, kila moja kati ya nchi hizo mbili, imetekeleza kwa ufasaha mipango muhimu ya kisiasa ya kitaifa, na kufungua zama mpya za uhusiano kati ya China na Russia.
Kwa upande wake Rais Putin, yeye ametuma salamu za kumtakia heri ya mwaka mpya Rais Xi, na kuwatakia furaha na afya njema raia wa China.
Mwaka 2019, China na Russia zitaadhimisha miaka 70 tangu zianzishe uhusiano wa kidiplomasia, Rais Putin amesema anaamini kuwa hiyo itakuwa fursa ya kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili na kuendelea kushughulikia masuala ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |