Kiwanda cha kuchinja na kusindika nyama wilayani Longido nchini Tanzania kinatarajiwa kuanza opaeresheni kabla ya Julai mwaka 2019.
Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuchinja mbuzi na kondoo kati ya 1000 na 2000 kila siku.
Mkuu wa wilaya ya Longido Frank Mwaisumbe amesema ujenzi wa mindo mbinu kwenye kiwanda hicho itakamilika hivi karibuni.
Amesema wafugaji wa eneo hilo ambao hutegemea mifugo kiuchumi ndio watakaofaidi zaidi kutokana na kiwanda hicho.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |