Kampuni moja ya china imesaini makubaliano ya kujenga hospitali kwa gharama ya dola milioni 47.8 katika kaunti ya Machakos nchini Kenya.
Kampuni hiyo ya Zhongcheng Import and Export Co imesaini makubaliano hayo na kampuni ya Lianard Holding kujenga hospitali hiyo itakayokuwa na vitanda 220 na nyumba za kulala 300.
Kwa sasa miradi ya kadhaa ya kujenga hospitali inaendelea huku serikali na sekta binafsi zikiwa mbioni kuziba mwanya uliopo.
Mapema mwaka 2018 chuo kikuu cha Nairobi na kampuni ya Guangzhou Cherami zilisaini makubaliano ya kujenga kituo cha kutibu saratani mjini Nairobi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |