Kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba anawakosea heshima na kuwakosesha raha wapinzani wake kwa jinsi anavyosherehekea kufunga mabao. Malalamiko hayo yametolewa na kiungo wa kati wa zamani wa Chelsea Claude Makelele. Pogba amekuwa akisherehekea kufunga mabao kwa kucheza ngoma, lakini Makelele anaamini amevuka mipaka. Amemshauri Pogba kwa kumwambia afanye hivyo katika chumba cha kubadilishia mavazi, na sio uwanjani. Makelele alikasirishwa sana baada ya Manchester United kushinda magoli 4-0, kisha Pogba kucheza ngoma mbele yake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |