Jumla ya waamuzi 18 wa Tanzania wameteuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), kuchezesha mechi za kimataifa kwa mwaka 2019. Katika orodha hiyo wapo waamuzi wa katikati na Waamuzi wasaidizi wa Kiume na wa Kike pamoja na waamuzi watakaochezesha mechi za soka ya Ufukweni. Waamuzi wenye beji za FIFA ni waamuzi wakuu, yaani waamuzi wa kati ambao ni wanne tu kwa upande wa wanaume, wakati sita ni waamuzi wasaidizi, maarufu kama washika vibendera.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |