Wafanya biashara kutoka jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo wamekataa kununua dagaa kutoka wilaya ya Pangani nchini Tanzania kufuatia kile wanachodai kuongezwa kwa ushuru. Wauzaji bidhaa hiyo kutoka Tanzania wameanza kulalamika kufuatia ukosefu wa soko.Baadhi ya wafanya biashara kutoka Tanzania wamesema wamekuwa wakinunua dagaa kutoka kwa wavuvi kabla ya kuziuza nchini DRC.Wafanya biashara hao walikuwa wakinunua dagaa gunia moja kwa shilingi elfu 20 lakini hivi sasa wacongo wamegoma baada ya kupandishiwa hadi shilingi elfu 330.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |