• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mashindano ya tenisi barani Afrika kutimua vumbi leo nchini Tanzania

    (GMT+08:00) 2019-01-08 09:38:00

    Mashindano ya tenisi kwa vijana Afrika, Tennis Zonal Championship, yanatarajiwa kuanza leo hadi januari 15, 2019 katika viwanja wa Gymkhana, jijini Dare es Salaam yakishirikisha jumla ya nchi 10.

    Rais wa chama cha tenisi Tanzania TTA, Denis Makoi amesema nchi zinazozishiriki ni Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Comoro, Sudan, Somalia, Ethiopia, Eritrea, Ushelisheli, pamoja na mwenyeji Tanzania.

    Aidha amesema TTA kwa kushirikiana na shirikisho la mchezo wa Tenisi Afrika (CAT) na shirikisho la Tenisi Duniani (ITF) wamejipanga vyema katika kuhakikisha mashindano hayo yanafanikiwa na timu bora kushinda, huku mazingira mazuri yameandaliwa kwa timu hizo kupata malazi mazuri kipindi chote cha mashindano.

    Mashindano hayo yatahusisha vijana wa umri wa miaka 14 na 16, na washindi watapata tiketi ya kushiriki mashindano ya tenisi ya Afrika mwezi Aprili mwaka huu, katika nchi za Afrika Kusini na Morocco.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako