Hii ni baada ya Safaricom kuzindua mpango wa Fuliza kwa watumiaji wote wa M-Pesa nchini.
Safaricom iliamua kuanzisha mpango huo baada ya kuufanyia majaribio Novemba mwaka 2018.
Watumiaji wa M-Pesa nchini Kenya ni 24.2 milioni na wanatarajiwa kunufaika na mpango huo mypa.
Kwa kutumia Fuliza, wateja watakuwa na uwezo wa kutumia hadi Sh50, 000 kulingana na kiwango wanachohitaji.
Kampuni hiyo inashirikiana na Benki ya KCB na CBA. Mteja akichukua, atalipa kwa riba ya asilimia 0.5 kwa siku.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |