• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda: Magari ya kawi ya jua kuanza kuzalishwa Uganda mwaka huu

    (GMT+08:00) 2019-01-11 20:15:27

    Waziri wa sayansi teknolojia na uvumbuzi wa Uganda Dkt. Elioda Tumwesigye amesema nchi hiyo itakuwa na mabasi yake yanayotumua kawi ya jua na kuhudumu katika barabara ya Kampala – Entebbe kabla ya mwisho wa mwaka 2019.

    Tumwesigye amewaambia waandishi wa habari kuwa serikali itaanza kufanyia majaribio mabasi hayo mwaka huu na kwamba serikali iko tayari kutoka shilingi bilioni 143 kusaidia utengenezaji wa magari nchini humo.

    Mwaka 2014 mamlaka ya uwekezaji ya Uganda ilitoa kandarasi kwa kampuni mbili - Kiira Motorinayomilikiwa na chuo kikuu cha Makerere na China Engineering kuanza uzalishaji wa magari mwaka 2018.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako