• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Bibi May kulihutubia bunge wakati siku ya upigaji kura kuhusu Brexit ikikaribia bungeni

    (GMT+08:00) 2019-01-15 09:02:30

    Waziri Mkuu wa Uingereza Bibi Theresa May amesema atatoa hotuba ya mwisho kwenye mijadala kuhusu hatma ya Uingereza kwenye Umoja wa Ulaya.

    Licha ya kuwataka wabunge kuunga mkono makubaliano aliyofikia na Umoja wa Ulaya, ni wachache wanaoona kuwa Bibi May ana uungaji mkono wa kutosha kati ya wabunge 640 wanaopiga kura leo jioni. Akishindwa kwenye upigaji kura huo kama inavyotarajiwa na wengi, Bibi May atatakiwa kuja na mpango mpya bungeni jumatatu ijayo.

    Kiongozi wa chama cha Labour Bw. Jeremy Corbyn amekutana na wabunge wa chama chake na kuwaambia kuwa kutakuwa na upigaji kura wa kutokuwa na imani na Bibi May.

    Wakati huo huo kiongozi wa walio wengi bungeni Bw Gareth Johnson, jana alijuzulu nafasi yake siku moja kabla ya kupiga kura. Mhafidhina huyo ameonya kuwa kama makubaliano ya Bibi May yakikataliwa huenda Uingereza isijitoe Umoja wa Ulaya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako