• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • ADAK yatoa rai kwa Wakenya kuzidisha vita dhidi ya pufya

    (GMT+08:00) 2019-01-16 08:36:15
    Shirika la kukabiliana na matumizi ya dawa za kusisimua misuli muchezoni nchini Kenya (ADAK) limetoa rai kwa wakenya kujitokeza kuunga mkono zaidi vita dhidi ya matumizi ya dawa hizo zinazojulikana zaidi kama pufya unaoiweka Kenya pabaya.

    Wito huo wa ADAK umetolewa siku chache baada ya rais wa shirikisho la riadha la Kenya (AK) Jackson Tuwei kuwasihi wanariadha kuachana na njia ya mkato ya kupata ufanisi ili kusafisha jina la nchi hiyo.

    Kwa masikitiko ameeleza kuwa Kenya inaelekea kupigwa marufuku na shirikisho la riadha duniani (IAAF) kutokana na watumiaji wa dawa hizo haramu mashindanoni kuongezeka.

    Mbali na Kenya, nchi zingine zinazotupiwa macho na IAAF ni Ethiopia, Belarus, India na Ukraine.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako