Liunda ameeleza kuwa tayari awamu ya kwanza ya ukaguzi kutoka kwa kamati maalum ya shirikisho la soka Afrika (CAF) umefanyika na wametoa maelekezo juu ya vitu vya kufanya kuelekea michuano hiyo.
Viwanja ambavyo vimepangwa kutumika katika michuano hiyo ni uwanja wa taifa, uwanja wa Uhuru na Uwanja wa Chamazi. Huku jumla ya timu 8 ikiwemo mwenyeji Tanzania zitashiriki michuano hiyo. Mataifa mengine ni Morocco, Senegal, Guinea, Nigeria, Cameroon, Uganda na Angola.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |