SOKA: Kane kukosa mechi 7 ikiwemo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
(GMT+08:00) 2019-01-16 08:37:00
Kwa mujibu wa ripoti ya madaktari, kuna uwezekano mkubwa kwa mchezaji wa Tottenham Hotspurs Harry Kane kukaa benchi kwa muda wa wiki 10 hali itakayopelekea kukosa mechi 7 kufuatia jeraha la goti alilolipata wakati timu yake ilipocheza na Manchester United.
Kane atakosa mechi kadhaa ikiwemo mechi ya ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Dortmund.