Palestina imechukua nafasi ya Misri na kuwa mwenyekiti mpya wa Kundi la 77 na China kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York. Kwa Mwaka huu Palestina itaongoza kundi hilo ambalo ni muungano wa nchi 134 zinazoendelea. Akipokea uenyekiti huo Rais Mahmoud Abbas wa Palestina amesema ni wajibu kwa taifa la Palestina kufanya kazi zake kwa unyenyekevu, udhati na kujitolea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |