Mwanasoka huyo sasa atajiunga na golikipa mahiri wa timu ya taifa Harambee Stars Patrick Matasi anayedakia timu hiyo na kocha wa zamani wa Sofapaka Steward Hall ambaye pia alikuwa mkufunzi wa Mieno alipochezea Batoto ba Mungu.
Kwingineko kiungo chipukizi wa Tanzania Said Hamis Ndemla leo anatarajiwa kuanza majaribio mafupi katika Klabu ya AFC Eskilstuna ya ligi kuu nchini Sweden.
Hiyo ni baada ya mchezaji huyo wa klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam kuwasili mjini Stockholm aiwa maeongozana na mshambuliaji mwingine chipukizi wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, Rashid Chambo wa JKT Ruvu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |