Msafara huo umepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini humo Luteni Jenerali mstaafu Paul Ignac Mella.
Balozi Mella amewatoa hofu viongozi na wachezaji wa Simba kuwa hali ya Kinshasa ni salama na hakuna vita wala hakutegemei kuwepo kwa vita.
Simba itakutana na AS Vita kesho Jumamosi, huku Simba ikiongoza kundi D kwa kuwa na Pointi tatu na magoli matatu ya kuifunga huku AS Vita haijapata pointi baada ya kukubali kipigo toka kwa Al Ahly ya Misri hivyo kukamata nafasi ya tatu katika msimamo wa kundi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |