Rais Donald Trump wa Marekani amemwambia spika Nancy Pelosi kuwa ziara yake ya nchi za nje imeahirishwa, siku moja baada ya bibi Pelosi kumtaka aahirishe hotuba yake kwa taifa kutokana na kuendelea kufungwa kwa baadhi ya idara za serikali. Rais Trump amesema safari za Bibi Pelosi za kwenda Brussels, Misri na Afghanistan zimeahirishwa na zitapangwa upya baada ya kumalizika kufungwa kwa serikali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |