Rais Donald Trump wa Marekani na makamu mwenyekiti wa kamati kuu ya Chama cha Wafanyakazi wa Korea Kaskazini Bw. Kim Yong Chol, watakutana ijumaa mchana katika Ikulu ya Marekani.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani Bibi Sarah Sanders amesema viongozi hao watajadili masuala ya kuondoa silaha za nyuklia na uhusiano wa pande mbili.
Mapema jana Bw. Kim alikutana na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Mike Pompeo, na wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilisema walikuwa na mazungumzo mazuri. Bw. Pompeo na Bw. Kim walikuwa wanatarajiwa kujadili tarehe na mahali utakapofanyika mkutano wa pili kati ya Rais Trump na Kiongozi wa Korea Kaskazini Bw. Kim Jong Un.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |