Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limetoa taarifa likisema watu 170 hawajulikani walipo au wamekufa kutokana na ajali za meli mbili zilizotokea hivi karibuni katika bahari ya Mediterranean.
UNHCR imesema taarifa za hivi karibuni kutoa shirika moja lisilo la kiserikali imesema watu 53 wamekufa katika bahari ya Abora lakini haikutaja muda wa ajali, ila mhanga mmoja ameokolewa baada ya kukwama baharini kwa saa 24, na kuokolewa na boti ya wavuvi, kwa sasa anapatiwa matibabu katika hospitali moja nchini Morocco.
Jeshi la majini la Italia pia limetangaza kuwa kuna ajali nyingine imetokea baharini, ambapo watu 117 wamekufa au hawajulikani walipo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |