Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR limeeleza kuhuzunishwa na habari kuhusu vifo au kutojulikana walipo kwa wahamiaji karibu 170, baada ya meli mbili walizokuwa wakisafiria kuzama kwenye bahari ya Mediterranean. Zaidi ya wahamiaji 2,200 wamefariki wakijaribu kuvuka bahari ya Mediterranean kuelekea Ulaya mwaka jana, na Libya ni nchi waliyotoka wahamiaji haramu wengi zaidi kutokana na hali ya kutokuwa na usalama na vurugu katika nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |