Pande hasimu mjini Tripoli, Libya zimefikia makubaliano ya kusimamisha vita baada ya upatanishi wa kikabila. Mkuu wa ujumbe wa upatanishi wa kikabila Mohamed al-Barghuthi amewaambia wanahabari kuwa pande hizo zitaondoa vikosi vyao kilomita 15 kutoka mpaka wa kila upandeļ¼ na silaha zote nzito na za kawaida. Pia amesema wamekubaliana kufungua barabara zilizofungwa na kuondoa vizuizi, kubadilishana wafungwa na mateka, kuhakikisha utekelezaji wa makubaliano na kusimamisha ulinzi wa kijamii na kijeshi na uungaji mkono kwa wahalifu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |