Chama cha mchezo wa Rga nchini Kenya kimethibitisha uteuzi wa Bi Sylvia Kamau kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa chama hicho. Bi Kamau ameteuliwa baada ya kujiuzulu kwa Ronald Bukusi mwezi Julai mwaka jana, moja ya majukumu yake ni kusimamia mchezo wa raga na mashindano kama vile Safari Sevens, mashindano ya kufuzu ya kombe la dunia kwa wachezaji wa chini ya miaka 15, kutafuta wadhamini na kuunganisha wadau wa mchezo huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |