Mwanariadha machachari nchini Kenya Geoffrey Kamworor ni miongoni mwa wanariadha watakaoshiriki shindano la riadha la taifa ya jeshi la polisi mwishoni mwa wiki hii siku ya jumamosi yatakayofanyika katika viwanja vya Ng'ong nje kidogo ya jiji la Nairobi.
Kamworor ambaye anashiriki mashindano hayo kwa mara ya kwanza amesema amejiandaa vyema na anamatumaini ya kuibuka mshindi katika mashindano hayo ya kilomita 10 kwa wakubwa. Mwanariadha mwingine Kaptagat atashiriki shindano hilo ikiwa ni kujiandaa kwa mashindano ya kimataifa yatakayofanyika mjini Aarhus nchini Denmark mwezi Machi mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |