Jeshi la Israel limeonya kuwa litafanya mashambulizi zaidi kama ghasia zitaendelea katika Ukanda wa Gaza. Jumapili jioni, jeshi la Israel lilifanya mashambulizi ya anga dhidi ya eneo la kaskazini mwa Gaza na kumwua mpiganaji wa kundi la Hamas mwenye umri wa miaka 24 na kuwajeruhi wengine wanne. Msemaji wa jeshi hilo amesema mashambulizi hayo ni ya kulipiza kisasi dhidi ya matukio ya ufyatuaji risasi karibu na uzio wa mpakani kati ya Gaza na Israel.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |