Idara ya Usalama wa Pwani ya Libya imesema jumla ya wahamiaji haramu 245 wakiwemo wanawake na watoto wameokolewa katika pwani ya magharibi ya nchi hiyo. Idara hiyo imetuma meli mbili kwenda kuwaokoa wahamiaji hao baada ya kupata ombi la msaada. Wahamiaji hao wanatoka nchi za Afrika na za kiarabu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |