Mawaziri wa biashara na viwanda wa Afrika wameelezea matumaini yao kuwa huenda utekelezaji wa soko huru la Afrika ukaanda katikati mwa mwaka huu.
Wamesema kuidhinishwa kwa makubaliano hayo kumeendelea kwa kasi huku wakitoa wito wa kuchukuliwa kwa hatua za utekelezaji.
Kamati ya kiufundi ya mawaziri hao imefanya mkutano kujadili mikakati ya bidhaa za Afrika, biashara ndogo na za wastani pamoja na uwezeshaji wa biashara.
Mapema mwezi ujao viongozi wan chi na serikali wanatarajiwa kwa mkutano wa Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia ambapo pamoja na maswala mengine wanatarajiwa kujadili soko huru la pamoja barani humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |