Zaidi ya watu 4,000 wamekwama kwenye kisiwa cha Kyotera nchini Uganda kutokana na ukosefu wa boti za kuwasafirisha.
Biashara kwenye vituo vya Kasensero na Kakuuto pia zimekwamba kutokana na tatizo hilo.
Uchukuzi uliathirika tangu Mei 2018 baada ya polisi wa idara ya uvuvi kuharibu boti za mbao ambazo wenyeji hutumia kusafiri.
Huduma za matibabu na nyingine za kibiashara kwenye kisiwa hicho cha karibu na mpaka wa Uganda na Tanzania zimezorota kwa miezi 7 sasa na wakaazi wanalazimika kutafuta huduma nchini Tanzania.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |