Makamu wa Rais wa China Bw. Wang Qishan akihutubia Mkutano wa mwaka 2019 wa Baraza la Uchumi Duniani WEF unaofanyika mjini Davos, Uswisi, ametoa wito wa kufanya kazi kwa pamoja kwa ajili ya kujenga mfumo wa kimataifa katika mapinduzi ya kiviwanda 4.0 unaolenga kujenga mustakabali mzuri zaidi kwa binadamu wote.
Bw. Wang Qishan amesema ni muhimu kuheshimu mamlaka ya kitaifa na kuacha kutafuta ubabe wa teknolojia na kuingilia kati mambo ya ndani ya nchi nyingine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |