Waziri wa habari, Sanaa, utamaduni na michezo wa Tanzania Dkt. Harrison Mwakyembe amesema Tanzania na nchi zingine za Afrika Mashariki zitajiulaumu endapo hazitajiandaa vyema kwa mashindano ya Olimpiki na Paraolimpiki yatakayofanyika mwakani nchini Japan.
Amesema wenyeji wa mashindano hayo Japan wamejitahidi kuandaa mazingira mazuri kwa ajili ya washiriki wa mashindano hayo, sasa ni muda wa Tanzania na Afrika mashariki kufanya vizuri na kunyakua medali.
Naye balozi wa Japan nchini Tanzania Shinichi Goto ameeleza kuwa Serikali ya Japan imejiandaa vizuri kwa ajili ya washiriki watakaokuwa katika kipindi chote cha mashindano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |