Watu 20 wakiwemo watoto wamefariki katika ajali ya barabarani iliyotokea jana mchana katika barabara kuu ya Ngaoundere hadi Touboro kaskazini mwa Cameroon. Mashuhuda wamesema ajali hiyo ilitokea wakati lori moja lilipogongana uso kwa uso na basi. Kwa mujibu wa abiria aliyenusurika, watu kadhaa wamejeruhiwa na wanatibiwa hospitali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |