Mchezo wa maruadiano wa nusu fainali ya kombe la ligi ya Uingereza maarufu kama Carabao ilipigwa jana uwanja wa Pirelli kwa timu ya Manchester City ilipokutana na Burton.
Man City imeshinda bao 1-0 lililofungwa na Sergko Aguero dakika ya 26 akimaliza pasi ya Riyad Mahrez na kufanikiwa kufuzu kwa jumla ya magoli 10-0 baada ya kushinda 9-0 kwenye mchezo wa kwanza. Nayo Chelsea imeifunga Tottenham Hotspurs kwa mabao 2-1 katika mchezo wa marudiano uwanja wa Stamford Bridge jijini London.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |