kufuatia ushindi huo, wadau mbalimbali walishindwa kuzuia mahaba yao, mchezaji wa ngumi kutoka Ireland Conor Anthony McGregory amemsifia kocha wa sasa wa Manchester United raia wa Norway, Ole Gunnar Solskjaer baada ya ushindi wa ugenini dhidi ya Arsenal mchezo uliochezwa wikiendi hii.
tangu Ole Gunnar akabidhiwe klabu ya Man U na kucheza mechi 8 hadi sasa amefanikiwa kushinda mechi zote huku wakifunga zaidi ya magoli 20.
Mechi zingine zilizochezwa mwishoni mwa wiki, ni Chelsea imeifumua Sheffield Wednesday goli 3-0, nayo Crystal Palace imeibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Tottenham Hotspur.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |