Gavana wa mji wa Jalalaqsi nchini Somalia Bw. Mohamad Nur Caga Jof amesema jeshi la Taifa la Somalia (SNA) limemwua ofisa mwandamizi wa kukusanya kodi wa kundi la al-Shabaab kwenye operesheni yake katika mji wa Jalalaqsi.
Askari wa jeshi la Somalia na wa tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia wameimarisha mapambano dhidi ya wapiganaji wa Al-Shabab katikati na kusini mwa Somalia, na kufanya operesheni za mfululizo ili kuwatimua wapiganaji wa kundi hilo lenye uhusiano na kundi la al-Qaida katika mkoa huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |