Waziri mkuu wa Syria Bw. Emad Khamis amesema serikali yake imesaini makubaliano ya muda mrefu ya ushirikiano wa kiuchumi na Iran. Kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika mjini Damascus pamoja na makamu wa kwanza wa rais wa Iran Bw. Eshaq Jahangiri, Bw. Khamis amesema makubaliano hayo ni ya kihistoria kwa ushirikiano wa aina mpya na Iran. Amesema makubaliano hayo yanahusu sekta za viwanda, kilimo, huduma, miundombinu, na nishati.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |