Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani Bibi Nancy Pelosi amemwalika rais Donald Trump kuhutubia taifa Februari, 5. Na rais Trump amekubali mwaliko huu. Awali Bibi Pelosi alimwalika Rais Trump kutoa hotuba yake bungeni Januari, 29, lakini baadaye alimtaka aahirishe hotuba yake kutokana na sababu za kiusalama, kwani idara za usalama hazikupewa pesa kutokana na kufungwa kwa baadhi ya idara za serikali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |