• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa Venezuela ailaani Marekani kwa kuweka vikwazo dhidi ya kampuni ya mafuta ya Venezuela

    (GMT+08:00) 2019-01-29 17:57:57

    Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ameilaani Marekani kwa kuweka vikwazo dhidi ya kampuni ya mafuta ya Venezuela, na kusema kitendo hicho kimekiuka sheria husika.

    Akizungumza kwa njia ya televisheni hapo jana, Rais Maduro amesema, kuweka vikwazo dhidi ya kampuni ya mafuta ya Venezuela na ofisi yake nchini Marekani ni kitendo cha uhalifu kinachokiuka sheria ya kimataifa na katiba ya Umoja wa Mataifa, kikiwa na lengo la kuiba mali ya Venezuela katika nchi nyingine, na serikali ya Venezuela itachukua hatua zote za kisheria ili kulinda mali yake ya kitaifa.

    Wakati huo huo, rais Maduro amesisitiza kuwa anapenda kufanya mazungumzo na chama cha upinzani ili kulinda utulivu na amani ya taifa, pia anapenda kufanya mawasiliano na serikali ya Marekani kama nchi hiyo ikikubali kutoingilia kati mambo ya ndani ya nchi nyingine.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako