Naibu waziri mkuu wa China na kiongozi wa mazungumzo kati ya China na Marekani Bw. Liu He ameongoza ujumbe wa China nchini Marekani kwa lengo la kufanya mazungumzo ya kiwango cha juu kuhusu masuala ya uchumi na biashara kati ya China na Marekani.
Ujumbe huo unajumuisha viongozi kadhaa wa serikali ya China akiwemo naibu mkurugenzi wa Kamati Kuu ya Maendeleo na Mageuzi Bw. Ning Jizhe, naibu waziri wa fedha Bw. Liao Min, na naibu waziri wa mambo ya nje Bw. Zheng Zeguang.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |