Kampuni ya madini ya taifa ya Tanzania STAMICO imesema kipaumbele chake kwa mwaka huu ni kutafuta fursa za kibiashara, kuendelea kuboresha uwiano wa mali na madeni, na kufikia matarajio ya wadau na wateja wake.
Kaimu mkurugenzi mtendaji wa STAMICO Bw. Sylvester Ghuliku amesema kupitia taarifa, kuwa kampuni hiyo itajitahidi kuleta mabadiliko kupitia masuluhisho ya kiuvumbuzi, huku ikiendelea kukuza uhusiano mzuri na jamii kwa njia ya kutimiza majukumu yake ya kijamii kupitia miradi mbalimbali.
Bw. Ghuliku amesema mwaka huu kampuni hiyo pia inatarajia kuimarisha uwezo wake wa kuongeza mapato.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |