Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya Bw. Ghassan Salame na naibu wake anayeshughulikia masuala ya kisiasa Bibi Stephanie Williams wamekutana na wazee na wawakilishi wa makundi ya kiraia ya mji wa Tawergha. Wamejadili mahitaji ya watu wa mji huo waliorudi mjini mwao baada ya kukimbia makazi kwa miaka mingi. Katika machafuko ya mwaka 2011, baadhi ya watu wa mji wa Tawergha wakishirikiana na vikosi vya aliyekuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi kupambana na waasi katika mji wa karibu, na walikimbilia miji mingine nchini Libya baada ya kupinduliwa kwa utawala wa Gaddafi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |